HABIBU A.SHABANI
Licha ya Kampeni kadhaa kufanywa dhidi ya maambukizi ya UKIMWI nchini Tanzania Ikiwemo ya “TANZANIA BILA UKIMWI INAWEZEKANA”lakini takwimu za mwisho za mwaka 2015 Chini ya TACAIDS zinaonesha kuwa maambukizi ya virusi vya Ukimwi nchini yaliongezeka kwenye kundi la vijana wenye umri wa miaka kati ya 19 mpaka 24 tofauti na ilivyokuwa miaka mitano iliyopita, ambako kundi lililokuwa limeathiriwa zaidi lilikuwa miaka kati ya 25 mpaka 34.
Pia licha ya kwamba kiwango cha maambukizi mapya ya virusi hivyo nchini kimeshuka kutoka asilimia 7 mwaka 2004 mpaka kufikia asilimia 5.3 mwaka jana, takwimu za baadhi ya mikoa ikiwemo Singida, Kigoma, Arusha, Mtwara, Kilimanjaro na Kagera zilionekana kuongezeka.
kuendelea kuandamwa na maambukizi hayo, ni kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo maendeleo na mwingiliano wa watu, mikoa ya Tanga na Manyara ndiyo yenye takwimu chache za maambukizi zikiwa na asilimia 4 pekee kwa mwaka 2015.
Huenda kushindwa kufanya vizuri kwa kampeni zilizopita kulichangiwa na mambo mengi ila kubwa zaidi ni mtu ambaye anatakiwa kufikisha ujumbe kwenye jamii, Jambo ambalo limeisukuma Mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM) kwa kushirikiana na Tume ya kupambana na UKIMWI nchini (TACAIDS) kumteua msanii mashuhuri wa nyimbo za asili nchini Mrisho Mpoto kuwa balozi wa kampeni ya Kili Challenge, ili kuhamasisha uchangiaji wa fedha kwa ajili ya kutunisha mfuko wa mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI.
BOFYA PICHA HAPA CHINI UONE PICHA ZA UCHI BONGO HASA USWAZI
DON'T FORGET TO LIKE THE PAGE IN ORDER TO GET NEWS UPDATES HAPPEN AROUND THE WORLD
Filed Under:
MUZIKI
on Jumamosi, 7 Mei 2016
Chapisha Maoni